August 13, 2026

Swahili Orthodox Chants & Teachings

Ili kwa nia moja tuungame: Baba, Mwana na Roho Mtakatifu; Utatu wa asili moja, na asiyetengana.

Sunday of St Gregory Palamas – 2nd Sunday of Great Lent



Hymns for Sunday 15th March 2020 Lyrics

Resurrectional Apolytikion, Tone 6

Angelic powers were in Your sepulchre,/ and those who guarded You became as men long dead;/ and standing there was Mary by Your tomb seeking / Your pure and sacred body,/ You despoiled hades; yet tempted not by him was You,/ You did meet the Virgin O life bestower./ O You who rose from the dead,/ glory to You O Lord.

Utukufu kwa Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu.

Apolitikio ya Mt. Grigori Mtenda-miujiza (Grigori Palama) – sauti ya nane (8)

Mwanga wa imani ya Kiothodoksi,/ mwamba imara / wa Kanisa na mwalimu wake,/ aliyejuzwa na Mungu,/ wewe ni pambo la watawa,/ jemadari asiyeshindwa wa wanatheolojia,/ Ee Grigori Mtenda-miujiza,/ na pendo la Thessaloniki,/ malaika wa neema,/ usikome milele kuomba kwa ajili,/ ya wokovu wa roho zetu.

Sasa na siku zote, hata milele na milele. Amina.

Theotokio ya ufufuo – sauti ya 8

Ee Mwema uliyezaliwa / na Bikira / kwa ajili yetu, na kuvumilia / mateso ya Msalaba / na ukanyakua / mauti kwa mauti, / na kuonyesha / kuonyesha* / ufufuo kwa sababu U Mungu. / Usiwaache hao / ambao / uliwaumba kwa Mkono Wako. / Ee Mwenye rehema, / uonyeshe / upendo Wako kwa wanadamu, / na kumpokea Mzazi-Mungu/ aliyekuzaa / anayetuombea Kwako. /. Na uwaokoe ambao // hawana kimbilio, Ee Mwokozi wetu.

Anavathmi – Sauti ya 6 (2nd Plagal/sauti 2b)

Nimekuinulia macho yangu / wewe uliye Mbinguni;/ nirehemu,/ ili niishi katika Wewe.
Utuhurumie sisi watupu,/ na ututayarishe kuwa vyungu vya kutumika.

Utukufu kwa Baba,/ na Mwana na Roho Mtakatifu.// Sasa na siku zote,/ hata milele na milele. Amina.

Katika Roho Mtakatifu / ni kusudi ya kuokoa vyote;/ akiwa anampulizia kadiri yake mtu,/ anamtoa katika vitu vya nchi,/ kumpa mabawa,/ na kumkuza na kumweka juu.

Prokimeno
Ee Bwana inua nguvu Yako,/ na uje kwa ajili ya wokovu wetu. X2

Mstari: Sikiliza, ewe mchungaji wa Israeli.

Ee Bwana inua nguvu Yako,/ na uje kwa ajili ya wokovu wetu.

Alleluia baada ya kusoma waraka – sauti ya sita (2nd Plagal/Sauti 2b)

Alleluia Alleluia Alleluia

Mstari: Aketiye mahali pa siri pa aliye juu, atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.

Alleluia Alleluia Alleluia

Mstari: Nitasema, Bwana ndiye kimbilio langu.

Alleluia Alleluia Alleluia

source